Monday, June 11, 2012

DJ FATTY WA XXL YA CLOUDS FM AKIKAMUA BIG BROTHER AFRICA JANA.

 

The 91 day reality super-series Big Brother StarGame, produced for M-Net’s AfricaMagic, is being screened live 24/7 on DStv 197 & 198. On Sunday 10 June South Africa’s Lee & Keagan and Namibia’s Junia & Jesica were randomly selected for nomination this week.  
For more information log on to www.africamagic.tv/bigbrother

NMB YAIPA SERIKALI GAWIO LA BILIONI 7.9

 


Waziri wa Fedha,Dk William Mgimwa  kwa niaba ya serikali amepokea sh 7.9 bilioni kutoka benki ya NMB ikiwa ni gawio  la serikali kwa mwaka 2011 kama ilivoidhinishwa katika mkutano wake mkuu uliofanyika Juni 2, 2012.Gawio hilo lilitokana na serikali kumiliki asilimia 31.8 ya hisa katika benki  ya NMB.

Akizungumza baada ya kupokea hundi hiyo jijini Dar es Salaam Dk. Mgimwa alisema, amefurahishwa  na benki ya NMB kwa utendaji wake kwa kuwa mwaka 2010 iliweza kutoa sh bilioni 5.7 “Benki ya NMB inaonyesha dalili nzuri ya utendaji wake kwa  kuwa ongezeko  hili la mwaka  2011 la sh bilioni 7.9 kwa serikali ni ongezeko zuri na fedha hii iliyotolewa na NMB  Imeweza kuichangia  Serikali baada ya kupata faida kwa kuwa ni nyingi sana na itasaidia kuwalipa wafanyakazi wengi ” alisema Dk.Mgimwa”

Aidha, aliipongez NMB katika juhudi zake za kuisaidia serikali kupitia shughuli mbalimbali za kupambana na umasikini na kuboresha maisha ya wananchi wenye  mahitaji. Alisema anathamini mchango wa NMB katika ukusanyaji wa kodi unaofanywa kupitia matawi yake yaliyosambaa Tanzania nzimai.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji  wa NMB, Bw. Mark Wiessing alisema  NMB itaendelea kuleta huduma nafuu za kifedha kwa jamii ya kitanzania katika maeneo  yote ya vijijini na mijini “NMB imeweza kufikia wateja wake nchi nzima,pia imeweza kulipa kodi kwa serikali,ndio maana NMB ni benki bora kwa Tanzania

Tukio hilo muhimu lilishuhudiwa na manaibu wawili wa wizara ya Fedha na Uchumi, Katibu mkuu wa wizara ya fedha na manaibu wake watatu, mweka hazina mkuu, wakuu wa wizara zingine pamoja na wafanyakazi wa NMB

WAZIRI WA HABARI AZUNGUMZA NA MAAFISA HABARI NA MAWASILIANO WA SERIKALI LEO JIJINI MWANZA

 

Waziri wa Habari, vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella  Mukangara akiongea na maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali leo jijini Mwanza.Pamoja na mambo mengine amewataka maafisa hao kuielimisha jamii kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo yanayofanywa na serikali kupitia vyombo vya habari. 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Seith Kamuhanda (mstari wa kwanza) akifuatilia mada  kuhusu changamoto zinazoikabili Tanzania katika kuhama kutoka mfumo wa Analojia  kwenda Digitali kufikia mwaka 2012 katika Kikao kazi cha Maafisa habari na Mawasiliano wa Serikali leo jijini Mwanza. Wengine wanaoonekana nyuma ni maafisa habari na Mawasiliano wa Serikali.
Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali wakifuatilia kwa makini hotuba  iliyokuwa ikitolewa na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo leo jijini Mwanza.
Waziri wa Habari, Vijana na Utamaduni Dkt. Fenella Mukangara (mstari wa kwanza katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa Wizara hiyo na maafisa habari na Mawasiliano wa Serikali  mara baada ya kufungua kikao kazi cha Maafisa Habari na Mawasiliano leo jijini Mwanza

Rais Kikwete awaapisha mabalozi Kumi Ikulu jijini Dar es Salaam leo.

 

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo amewaapisha mabalozi wapya kumi ambao wataongoza idara na kurugenzi mbalimbali katika Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Pichani Rais akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wapya aliowaapisha ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi.Kutoka kushoto walisimama mstari wa mbele ni Balozi Bertha Semu Somi,Balozi Hassan Simba Yahya, Balozi Vincent Joel Thomas Kibwana,Balozi Naimi Sweetie Hamza Aziz,Balozi Irene Mkwawa Kasyanju na Balozi Dora Mmari Msechu.Waliosimama nyuma kutoka kushoto ni Balozi Silima Kombo Haji,Balozi Celestine Joseph Mushy, Balozi Mbelwa Brighton Kairuki na Balozi Ramadhan Muombwa Haji(picha na Freddy Maro)

Rais Dkt.Jakaya Kikwete ashiriki kumuaga Muasisi wa CHADEMA Bob Makani katika viwanja vya Karimjee leo.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal pamoja na Mama Salma Kikwete leo waliungana na viongozi wa CHADEMA na viongozi wengine wa kitaifa kutoa heshima zao za mwisho kwa mmoja wa waasisi wa CHADEMA marehemu Bob Makani ambayepia aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini ikiwemo ya Naibu Gavana wa Benki kuu katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.(picha zote na Freddy Maro)
Rais Jakaya Kikwete akiteta jambo na mwenyekiti wa chama cha CHADEMA Mh. Freeman Mbowe wakati wa kuaga mwili wa Muasisi wa chama cha CHADEMA marehemu Bob Makani
Rais Dkt.Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal na Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe wakibeba jeneza la marehemu Bob Makani
Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitoa heshima za Mwisho
Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiteta jambo na mjumbe wa tume ya kukusanya maoni juu ya katiba Prof.Mwesiga Baregu katika viwanja vya Karimjee leo.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpa pole Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Wilbroad Slaa katika viwanja vya Karimjee kufuatia msiba wa muasisi wa Chama hicho Bob Makani

WANAFUNZI WA UDOM WAJITOLEA KUCHANGIA DAMU KWA HIARI.


Makamu Mkuu Wa Chuo Kikuu Cha Dodoma Prof Idris Kikula (Wa Pili Kushoto) akiwa amesimama wakati akimkaribisha mgeni rasmi ambaye ni  mkuu wa wilaya ya Dodoma Mjini Mh Lephy Gembe aliyeongozana na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa Wa Dodoma, Na Balozi Job Lusinde katika zoezi la kujitolea damu kwa hiari lililofanyika siku ya leo Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) na Kuandaliwa na Taasisi ya Wanafunzi wanaosoma Shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO)

Mgeni Rasmi ambaye pia ni Mkuu Wa Wilaya ya Dodoma Mjini Mh Lephy Gembe akitoa neno fupi kwa wanafunzi na wafanyakazi wa Chuo Kikuu Cha Dodoma waliofika katika Zoezi la Kujitolea Damu kwa Hiari lililofanyika Chuo Kikuu Cha Dodoma jana.
Baadhi ya wanafunzi wakiwa wamejitokeza katika zoezi la kuchangia Damu kwa hiari lililofanyika jana Chuo Kikuu Cha Dodoma(UDOM) na kuandaliwa na taasisi ya wanafunzi wanaosoma shahada ya kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma(UDOM)
Afisa Mahusiano wa Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) Bi Beatrice alipokua akitoa damu kwa hiari katika Zoezi la Kuchangia Damu kwa Hiari lililofanyika Chuo Kikuu Cha Dodoma jana huku Akishuhudiwa na Mshauri wa wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) Mh Manongi(Mwenye Miwani)
 Afisa habari wa Taasisi ya wanafunzi wanaosoma shahada ya kwanza ya sosoholojia aliyemaliza rasmi muda wake leo ambaye pia ni Mmiliki wa Mtandao wa LUKAZA BLOG Mh Josephat Lukaza akiwa tayari ameshamaliza zoezi la uchangiaji wa Damu kwa Hiari ambalo liliandaliwa na taasisi ya wanafunzi wanaosoma shahada ya kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO) zoezi lililofanyika jana Chuo Hapo.

 Makamu Mkuu Wa Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) Prof Idris Kikula akiaga wanafunzi na wafanyakazi waliojitoa katika zoezi la uchangiaji damu kwa hiari lililoandaliwa na taasisi ya wanafunzi wanaosoma shahada ya kwanza ya sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO) lililofanyika chuo hapo jana.Picha Zote Na Josephat Lukaza wa