Friday, June 15, 2012

AGONGWA NA TRENI NA KUFARIKI DUNIA,HUYU NDIO KIJANA JACKSON THOBIAS a.k.a KUSH ALIYEGONGWA NA TRENI

Na.Mwandishi wetu.

Kijana mdogo wa miaka 17, Jackson Thobias aliyekuwa akisoma kidato cha nne ESACS Academy, amefariki kwa kugongwa na treni maeneo ya kwao kipawa, aligongwa akiwa anasikiliza music kwa headphones huku akichati katika simu yake wakati akitembea kwenye reli.

Pamoja na mlio mkubwa wa treni, na juhudi za watu kumpigia kelele kuwa kuna treni inakuja nyuma yake, Jackson hakusikia.

Marehemu Jackson ndio aliye shinda kwenye Tokelezeiyer Inter-School concert iliyoandaliwa na group  ya Friends 4 Friends tarehe 12 may 2012, pia alishinda dougie competition  wakati 5select Event ya EATV ilipotembelea ESACS wiki mbili zilizopita.

Alikuwa ni kijana mwenye kipaji na ndoto nyingi katika umri mdogo wa miaka 17, Mungu aipumzishe roho ya marehemu Jackson Thobias kwa amani, Amen.

PICHA NA MATUKIO TOFAUTI NDANI YA TUZO ZA TASWA USIKU WA JANA DIAMOND JUBILEE


 

Rais wa TFF, Leodegar Tenga wa pili kulia akiwa na Jellah Mtagwa kushoto kwake


Familia ya ndondi


Wadau wa ndondi
Tedi Mapunda kulia na bosi wake 


Eiphraim Mafuru kulia


Maswahiba wa siku nyingi, Shaaban Mkongwe kulia akiwa Waziri Mahadhi


Beki wa Mtibwa Salum Swedi 'Kussi'


Kaburu kulia akikabidhi tuzo


Daud Salum 'Bruce Lee' kulia akikabidhi tuzo


Athumani Hamisi akikabidhi tuzo


Asha Baraka akikabidhi tuzo


Mafuru akikabidhi tuzo


Ridhiwani Kikwete kulia akiwa na Benny Kisaka kushoto, cheko la maana


Dioniz Malinzi kushoto akikabidhi tuzo


Kapombe akipokea tuzo ya Mwanamichezo Bora Chipukizi kutoka kwa Salim Amir


Mzee Matumla akimkabidhi Kaburu tuzo ya Emmanuel Okwi


Mwenyekiti wa RT, akimkabidhi tuzo Mwanahamisi Gaucho


Aggrey Morris kushoto akipokea tuzo ya Mwanasoka Bora wa mwaka 


Ally Choky akikabidhi tuzo


Mafuru akipakia msosi


Kim Poulsen kulia akiwa na nani sijui


Jamal Rwambow kulia na Kaburu wakati wa maakuli


Serengeti Beer inapokolea, mambo huwa hivi...


Mzee El Maamry akimkabidhi tuzo George Tarimo


Mzee Mwinyi akimkabidhi tuzo Adolph Rishard


Mzee Mwinyi akimkabidhi tuzo Peter Tino


Mzee Mwinyi akikabidhi tuzo


Waziri Mahadhi akimpokelea tuzo marehemu baba yake, Omar Mahadhi


Kaburu akimsaidia Kapombe kupokea tuzo ya Mwanamichezo Bora wa mwaka 2011 


Juma Pinto akikabidhi tuzo


Zena Chande na swahiba zake


Shaffih Dauda kulia, Amour Hassan na Michael Maluwe


Tullo Chambo na bosi wake


Akina nani sijui hawa


BIN ZUBEIRY kulia na Shaffih Dauda

SHOMARI KAPOMBE AIBUKA MCHEZAJI BORA WA 2011 TUZO ZA (TASWA) DIAMOND JUBILEE


 

Rais Mstaafu wa awamu ya Mzee Ali Hassan Mwinyi akimkabidhi Mchezaji bora wa mwaka kutoka timu ya Simba na Taifa Stars Shomari Kapombe tuzo yake ya mwanamichezo bora wa mwaka wa  katika tuzo za  zinazoandaliwa na chama cha waandishi wa habari za michezo TASWA  na kudhaminiwa na kampuni ya bia ya Serengeti zilizofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa  Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.

Shomari Kapombe pia amezawadiwa kitita cha shilingi milioni 12 kutoka kwa wadhamini wa tuzo hizo kampuni ya bia ya Serengeti kutokana na ushindi huo wa tuzo ya mwanamichezo bora wa mwaka
Shomari Kapombe mchezji bora wa mwaka akiwa katika picha ya pamoja na wadhamini wa tuzo hizo pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Simba huku akiwa ameshikilia tuzo yake na mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 12 za kitanzania  kulia ni Mkurugenzi mtendaji wa Serengeti Richard Wells, kushoto ni Mkurugenzi wa Mawasiliano SBL Teddy Mapunda na wa pili kutoka kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Simba Geofrey Nyange Kaburu

Mzee Ali Hassan Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa zamani wa timu ya taifa iliyofanikiwa kushiriki mashindano ya kombe la mataifa huru ya Afrika mwaka 1980 mara baada ya kuwakabidhi tuzo ya heshima usiku wa kuamkia leo
Mzee Ali Hassan Mwinyi akizungumza na kutoa nasaha zake katika utozji wa tuzo hizo.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Kampuni ya bia ya Serengeti SBL Teddy Mapunda akitoa shukurani zake mara baada ya kukamilika kwa utoaji wa tuzo hiyo usiku wa kuamkia leo.
Baba mwenye uzao wa mabondia Mzee Matumla kulia  akikabidhi tuzo ya mwanamchezo bora wa kigeni katika soka Emmanuel Okwi kwa Makamu Mwenyekiti wa klabu ya Simba Geofrey Nyange aliyepokea tuzo hiyo kwa niaba ya mchezaji huyo,
Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji la Zanzibar ZBC Omar Said Ameir akikabidhi tuzo ya mchezaji bora wa Tanzania katika soka Agrey Morris katika hafla hiyo.
Mchezaji wa zamani wa timu ya Coast Union ya Tanga na Timu ya taifa Salim Amir akikabidhi tuzo kwa mchezaji Shomari Kapombe
Mpiga picha wa siku nyingi Athmani Hamisi akikabidhi tuzo kwa mchezaji bora wa kiume katika mchezo wa VoliboMbwana Ally huku akisaidiwa na msaidizi wake

Mwenyekiti wa kamati ya Tuzo za TASWA Masoud Saanane akizungumza katika hafla ya utozi wa tuzo hizo usiku huu kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee.
Mkurugenzi wa kampuni ya bia ya Serengeti Bw. Richard Wells akizungumza katika hafla ya utoaji wa tuzo za mwanamichezo bora wa Tanzania