Monday, July 16, 2012

MANCHESTER UNITED NDIO MABINGWA WA SERENGETI FIESTA BONANZA DSM

 

Ilao Ejakait Meneja wa Uendeshaji upande wa mauzo kampuni ya bia ya Serengeti akikabidhi zawadi kombe kapteni wa timu ya mashabiki wa klabu ya Manchester United ya Uingereza katika bonanza la Serengeti Fiesta Soccer Bonanza lililofanyika jana kwenye viwanja vya Sigara TCC Chang'ombe jijini Dar es salaam ,baada ya timu ya mashabiki hao kuwafunga mashabiki wa timu ya Bacelona na kuchukua kombe hilo Bonanza hilo lilishirikisha mashabiki wa vilabu mbalimbali vya Ulaya, katikati ni Allan Chonjo Meneja wa bia ya Serengeti Lager na kulia ni Bahati Singh Joseph Mahawi meneja Mauzo wa Serengeti
;
Kapten wa timu ya mashabiki wa Manchester United akinyanyua juu juu kombe lao mara baada ya timu ya mashabiki hao kuwafunga mashabiki wa timu ya Bacelona na kuchukua kombe hilo kulia ni Ilao Ejakait Meneja Uendeshaji na  mauzo  kampuni ya bia ya Serengeti Allan  Chonjo Meneja wa bia ya Serengeti Lager
Mashabiki wa Manchester United wakishangilia kwa nguvu baada ya kukabidhiwa kombe lao.

Meneja mauzo wa kampuni ya bia ya Serengeti Joseph Mahawi akikabidhi kombe la mshindi wa pili timu ya mashabiki wa Barcelona jana kwa kapten wa timu hiyo Michael Mashoto mara baada ya kuchukua nafasi ya pili katika bonanza la Serengeti Fiesta Soccer Bonanza kwenye viwanja vya TCC Chang'ombe kwa kufungwa na Manchester United
Mashabiki wa Manchester United wakishangilia baada ya kuingia fainali.
Mashabiki wa Machester United wakiimba kwa furaha
Warembbo wa Chelsea walikuwepo kuwakilisha
Wachezaji wa timu za mashabiki wa Manchester United na Barcelona wakichuana vikali katika mchezo wao wa fainali ambapo Manchester United ilishinda mchezo huo.
Mchuano mkali ukiendelea kwenye viwanja vya TCC Sigara.
Mambo ya mnyama na burudani ileile
Vinywaji vilikuwa vya kutosha kama vinavyoonekana katika picha
Mashabiki wa timu ya Chelsea wakishangilia mara baada ya kuingia nusu fainali.
Wadau kutoka kampuni ya bia ya Serengeti nao walikuwepo kuhakikisha kila kitu kiko sawa kutoka kulia ni Kaisi, Bahati Singh Meneja Matukio na Promosheni Queen Sendiga Afisa wa Promosheni Kanda ya Dar es salaam na Ilao Ejakait Meneja wa Uendeshaji upande wa mauzo
Mdau Heavy D. akiwa amekaa chini hoi huku jua likimpiga vibaya baada ya kukata tamaa kabisa kutokana na timu yake ya Arsenal kutolewa mapema katika bonanza hilo hapa anaonekana kama vile analalamikia kitu

Mashabiki wa Barcelona wakishangilia baada ya kuchukua ushindi wa pili katika bonanza hilo

BAADA YA KULWA(YANGA) KUPIGWA 2-0: DOTO(SIMBA) NAE LEO ANYOLEWA 2-0 NA URA

 

 Derrick Walulya mchezaji wa timu ya URA FC kutoka nchini Uganda ambaye aliwahi kuchezea timu ya Simba pia ya Tanzania akimiliki mpira mbele ya Felix Sunzu mshabuliaji wa timu ya Simba katika mchezo wa kuwania kombe la Kagame linaloandaliwa na Shirikisho la Vyama vya michezo Afrika Mashariki CECAFA unaochezwa kwenye uwanja wa Taifa jioni hii mpaka sasa mpira umekwisha na timu ya URA imeifunga timu ya Simba magoli 2-0. magoli hayo yamefungwa na mchezaji Feni Ali wa URA FC.
 Waamuzi wakiongoza timu kuingia uwanjani tayari kwa kuanza mchezo huo.
Wachezaji wa timu za Simba ya Tanzania na URA ya Uganda wakisalimiana kabla ya kuanza kwa mchezo huo kwenye uwanja wa Taifa jioni hii.
 Watangazaji wa kituo cha televisheni cha Supersport cha Afrika Kusini wakitoa tathmini ya mchezo huo kabla ya timu hizo kukutana ambapo inaonyesha kuwa Simba mara nyingi imekuwa ikifungwa na URA FC wakati timu hizo zinapokutana katika michuano mbalimbali.
Mashabiki wa timu ya Simba wakiwa wamefurika katika uwanja wa Taifa kujionea timu yao ikicheza na Waganda URA FC. (Picha kwa hisani ya fullshangwe.blogspot.com)

YUSUPH MANJI NDIO BOSI MPYA WA YANGA - ASHINDA KWA ASILIMIA 97. SANGA MSAIDIZI WAKE.

Kwa mujibu wa tovuti ya klabu ya Yanga haya ndio matokeo kamili ya wagombea ni:

Nafasi ya Mwenyekiti:
Yusuf Manji (kura 1876)  97.0%,  John Jembele (kura 40) 2.6%, Edgar Chibura (kura 4) 0.24%

Nafasi ya Makamu Mwenyekiti:
Clement Sanga (kura 1948) 62.6%, Yono S Kevela (kura 475) 23%, Ayoub Nyenzi (kura 288) 14%

Nafasi ya Ujumbe: 
Abdallah Bin Kleb (kura 1942), Moses Katabaro (kura 1068), Aaron Nyanda (kura 922), Geroge Manyama (kura 682), Beda Tindwa (kura 391), Edgar Fongo (kura 295), Graticius Ishengoma (kura 247), Jumanne Mwamenywa (kura 251), Justine Baruti (610), Lameck Nyambaya (kura 425), Omary Ndula (kura 170), Peter Haule (441), Ramadhan Said (249), Yono Kivela (123)

kutokana na matokeo yalivyo hapo juu safu ya viongozi waliochaguliwa ni
Mwenyekiti: Yusuf Manji,
Makamu Mwenyekiti: Clement Sanga
Wajumbe: Abdallah Bin Kleb, Moses Katabaro, Aaaron Nyanda, Geroge Manyama