Monday, July 16, 2012

BAADA YA KULWA(YANGA) KUPIGWA 2-0: DOTO(SIMBA) NAE LEO ANYOLEWA 2-0 NA URA

 

 Derrick Walulya mchezaji wa timu ya URA FC kutoka nchini Uganda ambaye aliwahi kuchezea timu ya Simba pia ya Tanzania akimiliki mpira mbele ya Felix Sunzu mshabuliaji wa timu ya Simba katika mchezo wa kuwania kombe la Kagame linaloandaliwa na Shirikisho la Vyama vya michezo Afrika Mashariki CECAFA unaochezwa kwenye uwanja wa Taifa jioni hii mpaka sasa mpira umekwisha na timu ya URA imeifunga timu ya Simba magoli 2-0. magoli hayo yamefungwa na mchezaji Feni Ali wa URA FC.
 Waamuzi wakiongoza timu kuingia uwanjani tayari kwa kuanza mchezo huo.
Wachezaji wa timu za Simba ya Tanzania na URA ya Uganda wakisalimiana kabla ya kuanza kwa mchezo huo kwenye uwanja wa Taifa jioni hii.
 Watangazaji wa kituo cha televisheni cha Supersport cha Afrika Kusini wakitoa tathmini ya mchezo huo kabla ya timu hizo kukutana ambapo inaonyesha kuwa Simba mara nyingi imekuwa ikifungwa na URA FC wakati timu hizo zinapokutana katika michuano mbalimbali.
Mashabiki wa timu ya Simba wakiwa wamefurika katika uwanja wa Taifa kujionea timu yao ikicheza na Waganda URA FC. (Picha kwa hisani ya fullshangwe.blogspot.com)

No comments:

Post a Comment