Wednesday, June 6, 2012

Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki wala Kiapo

 

Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) leo wameapishwa rasmi kushika madaraka hayo huku Tanzania ikiwa na Wawakilishi tisa katika Bunge hulo.

Wabunge hao waliapa baada ya kupatikana Spika wa mpya wa Bunge hilo ambapo safari hii ikiwa ni Uganda kushika Uongozi huo wa Juu wa Bunge na Mwana Uchumi, Margareth Zziwa kuchukua nafasi hiyo.

Wabunge wote wa Tanzania katika Bunge la Jumuiya ya Mashariki waliokula kiapo hii leo ni pamoja na Mwenyekiti wa Wabunge wa Tanzania kwenye Bunge EALA, Alhaj Adam Omar Kimbisa na Katibu wake, Mh Shy-Rose SaddrudinBhanji.

Wengine ni Mhe. Anjela Charless Kizigha, Mh. Maryam Ussi Yahya,Mh.Nderkindo Perpetua Kessy, Dkt Twaha Issa Taslima, Mhe. Abdullah Ali Hassan Mwinyi, Mhe Bernard Musomi Murunyana Mhe. Charles Makongoro Nyerere na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta anaeingia kwa wadhifa wake wa Uwaziri.

Wabunge hao wameapisha pamoja na wabunge wenzao wa Kenya, Uganda, Rwanda na katika picha juu ni Waziri wa Afrika Mashariki na mbunge wa Urambo Mh Samwel Sitta akiapa katika bunge hilo jana jijini ArushaSOURCE: FATHER KIDEVU BLOG
Mbunge Shy-Rose Banji akila kiapo chake
Mh. Alhaji. Adam Kimbisa
Mhe. Anjela Charless Kizigha
Mhe Bernard Musomi Murunyana
Mh.Abdullah Alli Hassan Mwinyi 
Mh.Nderkindo Perpetua Kessy
Mh.Charles Makongoro Nyerere
Dkt Twaha Issa Taslima

USAJILI MAMBO YAMEIVA,YONDAN AZICHANGANYA SIMBA YANGA.

 

Leo hii klabu ya Yanga imetangaza kumsajili kinda raia wa Tanzania Kevin Patrick Yondan mwenye umri wa miaka 17,Yondan ambaye anacheza nafasi ya beki wa kati hajajulikana ametokea Klabu gani alizaliwa 9/10/1994.Mkataba wa Yanga na kinda huyo ni wa miaka miwili na unataraji kumalizika msimu wa 2013/2014.


hapa chini ni sehemu ya mkataba wa beki huyo na klabu ya Yanga yenye maskani yake mitaa ya Twiga na Jangwani.

Wakati huo huo Simba Sc imetangaza kumuongezea mkataba wa miaka miwili beki wake wa kati Kelvin Patrick Yondani, mkataba huo mpya ulisainiwa tangia mnamo 23/12/2011 ikiwa ni maboresho ya mkataba wa awali uliokua unafika kikomo mwishoni mwa mwezi uliopita yaani 31/05/2012. Yondani mwenye umri wa miaka 27 pia ni beki wa kimataifa wa Tanzania.


Kelvin Patrick Yondani

First name:Kelvin Patrick
Last name:Yondani
Nationality:Tanzania
Date of birth:10 October 1984
Age:27
Place of birth:

 Baadhi ya michezo ambayo Kelvin Patrick Yondani ameichezea timu ya Taifa ya Tanzania.

TareheNyumbanimatokeo Ugenini
2012-06-02Côte d'Ivoire
2 - 0
Tanzania
2012-05-26Tanzania
0 - 0
Malawi
2012-02-23Tanzania
0 - 0
Congo DR
2011-11-15Tanzania
0 - 1
Chad
2011-11-11Chad
1 - 2
Tanzania
2010-06-07Tanzania
1 - 5
Brazil
2010-01-04Tanzania
0 - 1
Côte d'Ivoire

BIN KLEB ARUDISHA FOMU YAKE NA MANJI JANGWANI


ABDALLAH Ahmad Bin Kleb amerudisha fomu yake ya kugombea Ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga, lakini inadaiwa alikuwa ana fomu nyingine tatu, ambazo inadaiwa kuwa ni za Yussuf Manji kugombea Uenyekiti, Isaac Chanji, Makamu Mwenyekiti, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakhim Masu. Pichani Bin Kleb akikabidhi fomu hizo.




Anaondoka

Warembo wa Miss Dar InterCollege watambulishwa Mafian lounge

 

Mratibu wa Shindano la  Miss Dar InterCollege Dina Ismail katika hafla ya kuwatambulisha warembo wa shindano hilo alisema kwamba warembo watakaoshiriki  wanaendeleza na mazoezi kwenye hoteli ya Lamada jijini Dar es Salaam chini ya ukufunzi wa Marylidya Boniface, huku kwa upande wa shoo wakinolewa na Bob Rich.

Alisema mpaka sasa warembo 15 kutoka vyuo vya Biashara (CBE), Uandishi wa Habari (DSJ) na Time, Ustawi wa Jamii na kile cha Usimamizi wa Fedha (IFM) wamesharipoti kambini.Dina aliwataja warembo hao kuwa ni pamoja na Hilda Edward, Nancy Maganga, Saada Seleman, Neema Nashon, Rose Muchunguzi, Fina Revocatus, Jane Augustino,Theresia Issaya na Natasha Deo.Taji la kitongoji hicho linashikiliwa na Rose Msuya kutoka IFM.

Kwa upande mwingine, mratibu huyo ameyaomba makampuni mbalimbali kujitokeza kudhamini shindano hilo ambalo linatarajiwa kuwa la aina yake na hasa ikizingatiwa kuwa washiriki wake wana vigezo vya hali ya juu.

“Tunaomba makampuni mbalimbali yajitokeze kudhamini shindano letu…mpaka sasa wadhamini tulionao ni pamoja na kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Redd’s, Lamada Hotel, Ndege Insurance, Dodoma Wine na Clouds Fm.
Mratibu wa Shindano la  Miss Dar InterCollege Dina Ismail akimuelekeza jambo mmoja wa wadau wa urembo huku warembo wakipozi kwa picha.
Warembo wa Miss Dar InterCollege wakiwamejipanga mbele ya wadau na wadhamini katika uzinduzi wa bendi ya SkyLight iliyofanyika  Mafian Lounge iliyopo Masaki, bendi hiyo inamilikiwa na mmoja wa wadhamini wao Ndege Insurance.
Shampeni ikifunguliwa kama ishara ya utambulisha wa warembo hao katika hafla ya kuwatambulisha iliyofanyika juzi kwenye klabu ya Mafian lounge jijini Dar es salaam