Tuesday, May 29, 2012

THOMAS ULIMWENGU KUTOENDA KUWAVAA AKINA KOLO TOURE

Zikiwa yamebaki masaa kadhaa kabla ya timu ya Taifa ya Tanzania kusafiri kwenda kuwavaa Ivory Coast - taarifa rasmi kutoka kambi ya timu hiyo zinasema kwamba mshambuliaji Tom Ulimwengu hatosafiri na timu hiyo. 

Ulimwengu, mshambuliaji chipukizi wa timu ya soka ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ameshindwa kupona maumivu ya kifundo cha mguu aliyopata akiwa kwenye mazoezi ya timu hiyo mwanzoni mwa wiki iliyopita.

Mbali na Ulimwengu Taifa Stars pia itakuwa bila ya kiungo wa kutumainiwa wa Yanga Nurdin Bakari ambaye pia ameshindwa kupona maumivu ya nyama za paja yaliyokuwa yanamkabili. Ulimwengu na Nurdin wote walikosa mchezo wa kirafiki ulioisha kwa sare ya bila kufungana dhidi ya timu ya Taifa ya Malawi uliochezwa Uwanja wa Taifa Jumamosi iliyopita.

No comments:

Post a Comment