Tuesday, June 5, 2012

ALI MAYAI NAYE NDANI YA WANAOTAKA UONGOZI MPYA YANGA.

Taarifa rasmi nilizozipata kutoka makao makuu ya klabu ya Yanga, ni kwamba wachezaji wawili wa zamani wa klabu hiyo Ally Mayay na Aaron Nyanda wameamua kuchukua fomu za kugombea ujumbe wa kamati ya utendaji katika uchaguzi unaokuja ndani timu hiyo.

Ally Mayay ambaye alikuwa mjumbe wa kamati hiyo kabla ya kujiuzulu baada ya kutokea kwa hali ya kutokueleweka katika uongozi uliopita, amesema yeye na Aaron wameamua kufanya hivyo baada ya kuona bado wana vitu vikubwa wanavyoweza kutoa kuisadia klabu yao kuwa katika mfumo wa kisasa utakayoiletea mafanikio timu yao.

No comments:

Post a Comment