Sunday, June 3, 2012

WAKAZI MBAGALA KIBONDEMAJI WALIA NA DIWANI WAO

 


 WAKAZI wa Kibondemaji Kata ya Mianzini wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam  wamemlalamikia diwani wa kata hiyo, Cecilia Macha (CCM), kwamba ni kikwazo  cha kata hiyo kukosa huduma muhimu kwa jamii ikiwemo Zahanati.
 Wakizungumza kwa nyakati tofauti na fullshangweblog.com leo, Wakazi hao walisema diwani akiwa ndiyo Mwenyekiti wa maendeleo wa Kata, tangu achaguliwe ameshindwa kuitisha mkutano wa aina yeyote, kujadili kero zinazo wakabili  wananchi wa mtaa huo.
Wananchi hao walisema  wanamlalamikia diwani huyo kwakuwa anatambuwa fika kero za mtaa huo, ambapo hakuna shule ya msingi wala sekondari hali inayowafanya watoto kusafiri zaidi ya kilomita 4 hadi sita kwa ajili ya kufuata shule.
Mmoja wa wakazi hao, Halima Juma alisema ukiachilia mbali kukosekana kwa shule, bado akina mama wajawazito wamekuwa wakipata matatizo makubwa kutokana na kukosekana kwa  barabara hali inayofanya usafiri kuwa wakubahatisha pindi wanapotaka kwenda hospitalini wakati  kujifungua.
"Angali  hakuna barabara, maji wala zahanati na kituo cha polisi huduma ambazo ni muhimu katika maisha ya kila siku kwa jamii"alisema Halima.
Naye Christopher John alisema  serikali inapaswa kumchukulia hatua mkandarasi aliyejenga barabara ya mtaa huo kwani ameijenga katika kiwango kisichoridhisha na kusababisha barabara hiyo kuharibika kwa muda mfupi.
Alisema barabara iliyopo hivi sasa imejengwa kwa nguvu za vijana wa mtaa huo ambapo hivi sasa wanachimba mitaro,  iliyojengwa na mkandarasi huyo, imejifukia katika kipindi cha mwaka mmoja tangu kujengwa.
Akijibu malalamiko hayo, diwani wa Kata hiyo, Cecilia alisema serikali haiwezi kujenga hospitali kila mtaa ila hizo ni propaganda "Chamsingi mwandishi  naomba ufike ofisini kwangu nikukonyeshe hali halisi"alisema Cecilia.
Aidha, alisema matatizo mengine yamekuwa yakichangiwa na fungu dogo la pesa za maendeleo zinazotengwa katika wilaya ya Temeke yenye kata 42

No comments:

Post a Comment