Monday, July 9, 2012

ZIARA YA NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI MARINE, TRL NA TPA MWANZA

 

Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dkt Charles Tizeba ,katikati akishuka kutoka katika meli ya Mv Victoria, mbele ni Kaimu Meneja wa kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) Projest Samson Kaija na nyuma ya Wasziri ni mkjuu wa Wilaya ya Nyamagana, Baraka Konisaga ‘Mtumishi wa Mungu.Tizeba alikuwa katika ziara ya siku moja akitembelea na kupata changamoto za watumishi wa kampuni za Reli (TRL), Huduma za Meli (MSCL) na Mamlaka ya Bandari (TPA) Mwanza .
PICHA NA MASHAKA BARTAZAR WA FULLSHANGWE-MWANZA


 Naibu wa Waziri wa Uchukuzi, Dkt Charles Tizeba akiongozwa na Kaimu Meneja wa Huduma za Meli (MSCL) Projest Samson Kaija, katikati.Kulia ni Meneja wa TPA Mwanza, Johnston Mutalemwa, kwenda kukagua hali ya meli ya Mv Victoria iliyokuwa imeegeshwa gatini baada ya safari ya Bukoba juzi.
  Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dkt Charles Tizeba wa pili kushoto, akielezwa jambo na  kaimu Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya reli (TRL), Kipallo Kisamfu wa kwanza kushoto, katikati mwenye shati jeupe ni DC wa wilaya ya Nyamagana, Baraka Konisaga, wa kwanza kulia ni Meneja Mamlaka ya Bandari (TPA) Johnston Mutalemwa, akifuatiwa na Afisa Mfawidhi wa Mamlaka ya udhibiti wa Usafiri wa vyombo vya majini na nchi kavu (SUMATRA) Alfred Waryana
Kaimu Meneja wa kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) Projest Samson Kaija , Kushoto wakimtembeza Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dkt Charles Tizeba ndani ya meli ya Mv Victoria , ili kujionea hali ya meli hiyo ilivyo mbapo aliagiza ifanyiwe ukarabati wa viti vya abiuiria ili kuwaezesha kusafiri kwa raha badala kuona kuwa usafiri wa meli hiyo ni karaha na wa shida.
Mmoja wa wachuuzi wa ndizi,ambaye hakutaka kutaja jina lake, akisubiri usafiri wa kusafirisha bidhaa hiyo kutoka bandari ya Mwanza kaskazini kwenda sokoni baada ya kupakuliwa kutoka ndani ya meli ya Mv Victoria juzi , kutoka mkoani Kagera.

Dkt Charles Tizeba, akizungumza na watumishi wa reli , mamlaka ya bandari na kampuni ya huduma za meli Mwanza, juzi katika ziara yake ya siku moja ili kujionea utendaji wa kamuni hizo za umma.

No comments:

Post a Comment