Tuesday, May 29, 2012

ALIYEKUWA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA WA ZAMANI, IDD SIMBA AFIKISHWA MAHAKAMA LEO NA WENZAKE 3

ALIYEKUWA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA WA ZAMANI, IDD SIMBA AFIKISHWA MAHAKAMA LEO NA WENZAKE 3

 Aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara wa zamani, Idd Simba akiongozwa na askari Polisi wakati alipofikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kujibu mashata 8 likiwemo la kula njama na, kughushi pamoja na kulitia hasara Shirika la Usafiri Dar es Salaam UDA zaidi ya Sh. milioni 300. Mshtakiwa huyo alifikishwa mahakamani hapo pamoja na washtakiwa wengeni watatu.
 Wakili Said Hamad El-Maamry (kushoto) akizungumza na Idd Simba Mahakamani hapo.
Mmoja wa watuhumiwa katika kesi hiyo, Aliyekuwa Diwani wa Sinza, Salim Mwaking'nda akiwa katika chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo mchana.

Na Mwandishi Wetu
Aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara katika Serikali ya awamu ya Pili, Idd Simba ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la UDA leo amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kujibu mashata 8 likiwemo la kula njama, kughushi, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu pamoja na kulisababishia hasara Shirika hilo ya zaidi ya Sh. bilioni 2.3

 Mshtakiwa huyo amefikishwa mahakamani hapo pamoja na washtakiwa wengine watatu ambao Mbali na Idd Simba ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya UDA ,wengine ni Mkurugenzi Salim Mwaking’inda na Meneja Mkuu wa shirika hilo, Victor Milanzi wa shirika hilo ambao wanatetewa na mawakili wa kujitegemea Alex Mgongolwa na Said El Mamry ambapo upande wa Jamhuri unawakilishwa na wakili wa Taasisis ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa,Ben Lincol.

No comments:

Post a Comment