Tuesday, June 5, 2012

EURO 2012: SPAIN - JE WATAWEZA KUWEKA REKODI YA KUBEBA TAJI LA TATU MFULULIZO AU WATAFUATA NYAYO ZA UFARANSA KWENYE WORLD CUP 2002?

Ufaransa ndio ilikuwa nchi ya mwisho kwenda kwenye michuano mikubwa ya kimataifa kama mabingwa wa dunia na ulaya, lakini jitihada za kuwa taifa la kwanza kushinda 'treble' makombe matatu mfululizo  katika historia ya soka la kimataifa zilishindikana kwa aibu , baada ya kumaliza kwenye nafasi ya mwisho kwenye kundi A katika michuano ya kombe la dunia mwaka 2002.

Spain wanajaribu kutengeneza historia kwenye kipindi hiki cha kiangazi. Ingawa maandalizi yao yamekuwa yakiwekwa kwenye wakati mgumu kutokana na majeruhi ya Carles Puyol na David Villa,  huku kukiwa na mashaka juu ya form ya Fernando Torres na hali ya kuwa fiti kwa kiungo Xavi Hernandez, kuonekana kutokuwepo kwa hatari yoyote ya kuwatokea kwa aibu ya kutolewa kwenye hatua ya makundi na kurudia historia ya aibu ya wafaransa iliyotokea miaka 10 iliyopita.

Spain kwa sasa wapo katikati ya kizazi chao cha dhahabu: wameshatengeneza na kui-master style yao ya uchezaji, kukava kila sehemu ya dimba, huku wakiwa na mazao ya vipaji vipya (Jordi Alba na wenzie) na vya zamani Xavi na kundi lake, Spain ndio ya kuogopwa zaidi kwenye michuano ya Euro.

Nahodha na golikipa Iker Casillas alisema timu yao inakumbuka sana kipigo walichopewa na Switzerland kwenye mchezo wao wa ufunguzi kwenye WOZA 2012, na sasa wamejipanga kupata suluhisho la namna ya kucheza na kupata matokeo dhidi ya timu ambazo zinapenda kupaki basi golini. Huku Italy na Ireland wakiwa ndio wapinzani wao kwenye mechi zao mbili za mwanzo katika kundi C, Spain watahitaji kupata mbinu mbadala ya kucheza dhidi ya wapaki mabasi.
Kutoka kwa Shaffihdauda.com

No comments:

Post a Comment