Friday, June 8, 2012

HEKAHEKA YA USAJILI YANGA KUFURU MWAKA HUU MAXIMO ATUA JUMA 4 KUZUNGUMZA NAO.

Baada ya kufanya vibaya katika msimu uliopita, Yanga wameendelea kuunda timu upya, baada ya juzi kumsainisha Kelvin Yondan, leo hii timu hiyo imehamia kwenye benchi la ufundi.

Taarifa za kuaminika kutoka ndani ya zinasema klabu hiyo imemtumia tiketi ya ndege kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Tanzania, Marcio Maximo kwa ajili ya kuja kufanya mazungumzo ya kujiunga na klabu hiyo kwa ajili ya kuliongoza benchi la ufundi la wanajangwani kuanzia msimu ujao.

"Mpaka sasa tumefanya mazungumzo ya awali na Maximo na tumefikia makubaliano ya kimsingi, ambayo tunaweza kuja kuyakamilisha hapa nchini atakapotua siku ya jumanne wiki ijayo." - kilisema chanzo hicho cha kuaminika.

No comments:

Post a Comment