Sunday, June 3, 2012

TAIFA STARS YAJIPANGA KUIKABILI GAMBIA NYUMBANI


Kikosi cha Taifa Stars ambacho jana kilicheza na Ivory Coast hapa Abidjan na kupoteza kwa mabao 2-0 kinaendelea kujinoa kwa mechi ijayo dhidi ya Gambia itakayochezwa Jumapili (Juni 10 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
 
Kwa mujibu wa programu ya Kocha Kim Poulsen, Taifa Stars imefanya mazoezi leo asubuhi kwenye uwanja wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Ivory Coast (FIF) ambao uko pembezoni mwa jiji la Abidjan.
 
Timu hiyo itafanya tena mazoezi kesho (Juni 4 mwaka huu) asubuhi kabla ya kuanza safari ya kurejea nyumbani saa 1.30 usiku kwa ndege ya Kenya Airways kupitia Nairobi ambapo itawasili Dar es Salaam, Juni 5 mwaka huu saa 1.40 asubuhi.

No comments:

Post a Comment