Tuesday, June 5, 2012

LULU KUFIKISHWA TENA MAHAKAMANI JUNI 18

 

Mwigizaji wa filamu, Elizabeth Michael 'Lulu' anayekabiliwa na kesi ya kumuua mwigizaji mwenzake, Steven Kanumba, akisindikizwa na askari Magereza kuingia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, kwa ajili ya kusomewa mashitaka  yake. Kesi hiyo imehairishwa hadi juni 18. (PICHA NA DOTTO MWAIBALE)

KESI ya mauaji inayomkabili msanii wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ imeahirishwa hadi Juni 18 mwaka huu,  kwa sababu upelelezi wa shauri hilo bado haujakamailika.

Wakili wa Serikali Peter Sekwao alidai kuwa kesi hiyo imekuja kwa kutajwa, pia alidai kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

Baada ya kudai hivyo Hakimu Mkazi , Agustina Mmbando wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam aliahirisha kesi hiyo hadi Juni 18 mwaka huu, ambapo itakuja kwa kutajwa.

Awali  Mei 7 mahakama hiyo ilitupilia mbali ombi la mawakili wa upande wa  utetezi katika kesi inayomkabili Lulu kuwa mahakama
 imuone ana miaka chini ya miaka18.

No comments:

Post a Comment